KIUNGO
mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Simba Madaraka Selamani,timu za
Chile na Mexico,zili staili kucheza fainali za kombe la dunia za mwaka
huu kutokana na kiwango walichoonesha.
Madaraka aliyewahi kuichezea klabu ya Simba kwa mafanikio makubwa
ikiwemo kuibebesha ubingwa wa Tanzania bara mara tatu,alizitaka timu za
Afrika kuiga mfano wa timu hizo kutokana ushindani waliouonyesha licha
ya kutolewa katika hatua ya mtoano.
“Timu za Afrika zinapaswa kuiga mfano wa timu za Chile na
Mexico,ambazo hazikuwa na wachezaji wenye majina makubwa lakini
zilionyesha ushindani wa kweli na kuwatoa jasho waandaji wa fainali hizo
Brazili,”alisema Madaraka.
Mkongwe huyo pia alisema haipi nafasi Brazili ya kunyakua ubingwa huo
kwa sababu imeonyesha kuwa na mapungufu mengi licha ya kufika hatua
hiyo ya robo fainali.
“Hii siyo Brazili ile ambayo tulikuwa tunaifahamu ambayo huiwezi
kumaliza dakika 90, pasipo kutikisa nyavu za wapinzani tumeshuhudia
mechi mbili ile ya
Showing posts with label Michezo. Show all posts
Showing posts with label Michezo. Show all posts
Sunday, 6 July 2014
Thursday, 2 May 2013
BREAKING NEWS: FIFA YAWARUDISHA WAMBURA NA MALINZI
Malinzi, Wambura warudishwa kugombea TFF na FIFA.
Jamal Malinzi na Michael Wambura wamerudishwa kuwania nafasi walizokuwa
wakipigania kuzipata katika uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Soka
Tanzania (TFF).
Kuna taarifa kwamba wagombea wawili, Jamal Malinzi na Michael Wambura wamerudishwa kuwania nafasi walizokuwa wakipigania kuzipata katika uchaguzi mkuu wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF).
Thursday, 11 April 2013
SAKATA NA KUFUNGIWA KOCHA BILAL LACHUKUA SURA MPYA
Ikiwa ni ni takribani siku tatu tu baada ya kamati ya ligi
ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania-TFF kumfungia kocha msaidizi wa Toto
African ya Mwanza Athumani Bilal mechi tatu kwa kosa la kumshambulia kwa maneno
kocha mkuu wa timu ya TZ Prisons Jumanne Challe sakata hilo limechukua sura
mpya.
Akizungumza na kipindi cha michezo cha Afya Radio 96.8mhz
kocha Athumani Bilal amekana ‘kumtukana ‘ kocha Jumanne Challe wa Tz Prisons anasema, ‘TFF nawashangaa sana sijamtukana na
siwezi kabisa kumtukana mwalimu wangu aliyenifundisha kazi Jumanne Challe na
pia siwezi kabisa kumtukana mtu yeyote Yule,ningekuwa nimemtukana ingewezekana
vipi baada ya mechi tuwe wote!?’ Anahoji Bilal na pia mbona sijahojiwa na mtu
yeyote au chombo chochote wanaishia tu kuhukumu ndo kazi zinavyofanyika hivyo?
Michezo na Afya ilipotaka kujua kilichosababisha yeye
kutolewa kwenye benchi la ufundi Bilal alijibu mpaka sasa sijui na sijui hata Yule
kamisaa aliandika nini kwenye ripoti yake.

Tuesday, 9 April 2013
SIR ALEX AZUNGUMZIA GEMU YA JANA
Sir Alex Ferguson amedai Manchester
United walikosa ‘bahati’ kwa kufungwa 2-1 na Manchester City hapo jana
na pia alikiri kuwa, Siku zote, Timu yake ‘hujibebesha zigo’ badala ya
kurahisisha kazi.
Ingawa jana walifungwa, Man United bado wapo kileleni wakiwa Pointi 12 mbele ya Man City na Mechi zikiwa zimebaki 7.
Kwa hali ilivyo sasa, Man United
wanahitaji kushinda Mechi 3 na Sare 1 kati ya hizo Mechi zao 7 ili
watwae Ubingwa ikiwa Man City watashinda Mechi za mbele yao.
TFF YATOA ADHABU KWA KLABU NA MAKOCHA VPL
KLABU ya Yanga na Kocha Msaidizi wa timu
ya Toto Africans, Athuman Bilali wamepigwa faini ya sh. 500,000 kila
mmoja kutokana na makosa mbalimbali katika mechi za Ligi Kuu ya Vodacom
(VPL) inayoendelea nchini.
Adhabu hizo zimetolewa na Kamati ya Ligi
ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) iliyokutana Jumapili
(Aprili 7 mwaka huu) jijini Dar es Salaam kupitia ripoti za waamuzi na
makamishna kwa michezo namba 108 hadi 171.
KAMATI YA TFF YAZIPONGEZA ASHANTI, MBEYA CITY, RHINO
Kamati ya Ligi ya Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) imezipongeza timu za Ashanti United ya Dar es
Salaam, Mbeya City ya Mbeya na Rhino Rangers ya Tabora kwa kupanda Ligi
Kuu ya Vodacom (VPL) msimu ujao (2013/20114).
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Wallace Karia
amezitaka timu hizo kufanya maandalizi ya kutosha ili ziweze kushindana
katika VPL ikiwemo kutimiza masharti ya kuwa klabu za Ligi Kuu.
PATASHIKA YA KUJINASUA KUSHUKA DARAJA KESHO
Polisi Morogoro inapambana na Ruvu
Shooting katika moja kati ya mechi tatu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL)
zitakazochezwa kesho (Aprili 10 mwaka huu). Matokeo ya mechi hiyo
yanatarajia kutoa mwanga kama Polisi inaweza kubaki kwenye ligi hiyo
msimu ujao.
Timu hiyo itakuwa nyumbani Uwanja wa
Jamhuri mjini Morogoro katika mechi hiyo itakayochezeshwa na Ibrahim
Kidiwa kutoka Tanga akisaidiwa na Godfrey Kihwili na Ephrony Ndissa wa
Arusha.
Polisi Morogoro inayonolewa na Adolf
Rishard inakamata nafasi ya mwisho ikiwa na pointi 18 tu na imebakiza
mechi tatu dhidi ya Simba, Kagera Sugar na Coastal Union.
Mechi nyingine za kesho ni kati ya
Tanzania Prisons iliyo nafasi ya 12 ikiwa na pointi 20 dhidi ya Mgambo
Shooting. Mwamuzi Hashim Abdallah wa Dar es Salaam ndiye atakayechezesha
mechi hiyo kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine jijini Mbeya. Mgambo
ina pointi 24 na iko katika nafasi ya tisa.
Mwamuzi Said Ndege wa Dar es Salaam
atachezesha mechi kati ya wenyeji Mtibwa Sugar na Toto Africans
itakayofanyika Uwanja wa Manungu ulioko Turiani mkoani Morogoro. Toto
Africans ya Kocha John Tegete ina pointi 21 ikiwa nafasi ya 11 wakati
Mtibwa Sugar iko nafasi ya tano na pointi zake 32.
Ligi hiyo itaendelea keshokutwa (Aprili
11 mwaka huu) kwa mechi moja kati ya Azam na African Lyon itakayofanyika
Uwanja wa Azam Complex.
Monday, 8 April 2013
TAKUKURU yawasafisha wachezaji Azam
TAKUKURU YAWASAFISHA WACHEZAJI WA AZAM
AMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
TAASISI YA KUZUIA NA KUPAMBANA NA RUSHWA
S. L.P. 42325,
Temeke,
Simu: 022 2850633,
Nukushi: (022) 2850635,
Baruapepe:rbctemeke@pccb.go.tz ,
Mtandao www.pccb.go.tz
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
UCHUNGUZI WA WACHEZAJI WA TFF
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) inatoa taarifa kwa
umma kwamba, uchunguzi uliofanywa na TAKUKURU Mkoa wa Temeke dhidi ya
wachezaji wanne wa timu ya soka ya AZAM waliokuwa wakituhumiwa kupokea
hongo/rushwa ili kupanga matokeo, haukuweza kuthibitisha tuhuma hiyo.
Subscribe to:
Posts (Atom)







