Thursday 11 April 2013

SAKATA NA KUFUNGIWA KOCHA BILAL LACHUKUA SURA MPYA



Ikiwa ni ni takribani siku tatu tu baada ya kamati ya ligi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania-TFF kumfungia kocha msaidizi wa Toto African ya Mwanza Athumani Bilal mechi tatu kwa kosa la kumshambulia kwa maneno kocha mkuu wa timu ya TZ Prisons Jumanne Challe sakata hilo limechukua sura mpya.
Akizungumza na kipindi cha michezo cha Afya Radio 96.8mhz kocha Athumani Bilal amekana ‘kumtukana ‘ kocha Jumanne Challe wa Tz Prisons  anasema, ‘TFF nawashangaa sana sijamtukana na siwezi kabisa kumtukana mwalimu wangu aliyenifundisha kazi Jumanne Challe na pia siwezi kabisa kumtukana mtu yeyote Yule,ningekuwa nimemtukana ingewezekana vipi baada ya mechi tuwe wote!?’ Anahoji Bilal na pia mbona sijahojiwa na mtu yeyote au chombo chochote wanaishia tu kuhukumu ndo kazi zinavyofanyika hivyo?
Michezo na Afya ilipotaka kujua kilichosababisha yeye kutolewa kwenye benchi la ufundi Bilal alijibu mpaka sasa sijui na sijui hata Yule kamisaa aliandika nini kwenye ripoti yake.




Michezo na Afya haikuishia hapo iliamua kumtafuta kocha Jumanne Challe:-
Mtangazaji: Hallow kocha,unaongea na Michezo na Afya Radio kutoka MWZ TZ, habari ya kazi?
Challe: Safi Mungu anasaidia kazi inaenda vizuri na tunaendelea kuhakikisha timu yetu haishuki daraja.
Mtangazaji: ok vizuri,kocha ni kwanini kocha Bilal alikutukana?
Challe: Bilal anitukane mimi! (kwa mshangao)
Mtangazaji: Bilal kafungiwa na TFF kwasababu alikutukana siku mlipocheza na Toto Mwanza.
Challe: sijawahi kutukanwa na Bilal na kwa nini anitukane,sasa kama alinitukana mbona baada ya mchezo tulikuwa wote kwa muda mrefu sana tukipiga stori mbalimbali (kwa sauti ya kuhoji na mshangao).
Mtangazaji: Asante kwa ushirikiano wako
Challe: asante na wewe na kazi njema.
Kocha Athumani Bilal amesema anakusudia kukata rufaa kwenye kamati ya rufaa ya TFF na pia anataka aombwe msamaha sababu suala hilo anasema limemshushia hadhi yake kwenye jamii.

0 comments:

Post a Comment