Thursday 11 April 2013

HILI NI JANGA


HII RIPOTI IMENISIKITISHA SANA

Wasichana wa Nzovwe jijini Mbeya wanapenda kupigwa 'mtungo'

WASICHANA wa eneo la Nzovwe, jijini Mbeya wametuhumiwa kushinda katika klabu za kuuza pombe za kienyeji, hasa nyakati za usiku na kufanya mapenzi na wanaume zaidi ya mmoja kwa siku kwa tamaa ya fedha.

Imedaiwa tabia ya wasichana hao, kupenda kuomba fedha kwa wanaume tofauti wanaokuwa wanakunywa pombe katika klabu hizo, hupelekea mwisho wa siku wakubali kufanya ngono zembe na mwanaume zaidi ya mmoja.

Hayo yalisemwa kwa nyakati tofauti na wakazi wa eneo hilo, katika mkutano wa hadhara ulioandaliwa na Vijana Mabalozi Watanzania wanaoishi na virusi vinavyosababisha Ukimwi (TAYOPA).

Mkoa wa Mbeya ni wa nne kutembelewa na TAYOPA ambao wapo kuutambulisha mradi wao uitwao 'Vijana Tuzinduke ili kujikinga na Ukimwi'.

Mikoa mingine iliyotembelwa ni Dar es Salaam, Lindi, Mtwara na baadaye wataelekea Ruvuma.
Mradi huo unafadhiriwa kwa pamoja na na shirika la Afya la Kimataifa (FHL) na kituo cha televisheni cha MTV cha nchini Marekani.

Wakizungumza wakazi hao wa Nzovwe walisema kuwa wasichana wa kike wa maeneo hayo, wamekuwa wanaendekeza sana kuombas fedha kwa wanaume katika klabu za pombe nyakati za usiku hali inayopelekea kuwepo kwa ngono zembe na wanaume wengi kwa siku.

Mkazi aliyejitambulisha kwa jina moja la Joyce alisema hali hiyo imefanya wasichana hao ambao bado ni wanafunzi wa shule za msingi, kupenda kufanya ngono na wanaume wengi mtindo ambao ni maarufu zaidi kwa jina la 'Mtungo'.

"Huku unaweza kumuona msichana ukadhani ni mdogo, kumbe anao uwezo wa kufanya mapenzi na zaidi ya mwanaume mmoja kwa siku...kimsingi hali inatisha kwani huwa wanafanya ngono zembe".Joyce alisema

Naye Mwenyekiti wa TAYOPA, John Solanya, alisema yeye alipimwa afya na kugundulika kuwa na maambukizi ya virusi vya Ukimwi tangu mwaka 1995, ambapo alijitangaza.

Solanya alisema kuwa anaishi na mke pamoja na mtoto mmoja ambao hawajaambukizwa Ukimwi, na kuwa tangu mwaka huu hajawahi kuumwa hadi kufikia hatua ya kulazwa hospitalini kwani amekuwa anazingatia ushauri anaopewa.

"Nina mke na mtoto ambao wao hana maambukizi ya Ukimwi... ninapotaka 'chakula cha usiku' kutoka kwa mke wangu huwa tunatumia kondomu" alisema Solanya.

Naye Fitina Mohamed, ambaye pia anaishi na virusi vya Ukimwi, alisema ni wengi wanayo maambukizi ya ugonjwa huo lakini huwezi kuwatambua kwa kuwaangalia kwa macho bali hadi wapime na kujitangaza.

Alihoji kuwa ni nani ambaye angeweza kuwatambua kuwa yeye ama mwenzake Solanya wanaishi na virusi vya Ukimwi iwapo wangeamua kukaa kimya mara baada ya kupima afya zao, na kuendelea kukubali kufanya ngono zembe.

Tukio hilo lilipambwa na burudani kutoka kwa wasanii Fareed Kubanda 'Fid Q. na mshindi wa Bongo Star Search, Jumanne Idd ambao waliweza kutoa burudani kabambe na kuwa kifutio kikubwa katika mkutano huo. 
NZOVWE ndo sehemu niliyokulia naweza kuwa shuhuda wa mambo jinsi yanavyokwenda ila sikuwahi kufikiria kama hali inaweza kufika hapo ilipofika sasa.BLOGGER wa Blog hii nina maslahi binafsi na Nzovwe so siwezi kukaa kimya kutokana na ripoti ya huu utafiti.Lazima hatua za haraka zifanyike ili kuokoa kizazi cha sasa na kijacho.
 Stori hii ilitoka mwezi wa kumi na mbili  source-www.jamiiforums.com  nimeamua kuirudia ili kutafuta njia za kuokoa jamii maana mimi naona hili ni JANGA

0 comments:

Post a Comment