Sunday 6 July 2014

Chile na Mexico hawakustahili kutolewa mapema Kombe la Dunia

KIUNGO mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Simba Madaraka Selamani,timu za Chile na Mexico,zili staili kucheza fainali za kombe la dunia za mwaka huu kutokana na kiwango walichoonesha.
Madaraka aliyewahi kuichezea klabu ya Simba kwa mafanikio makubwa ikiwemo kuibebesha ubingwa wa Tanzania bara mara tatu,alizitaka timu za Afrika kuiga mfano wa timu hizo kutokana ushindani waliouonyesha licha ya kutolewa katika hatua ya mtoano.
“Timu za Afrika zinapaswa kuiga mfano wa timu za Chile na Mexico,ambazo hazikuwa na wachezaji wenye majina makubwa lakini zilionyesha ushindani wa kweli na kuwatoa jasho waandaji wa fainali hizo Brazili,”alisema Madaraka.
Mkongwe huyo pia alisema haipi nafasi Brazili ya kunyakua ubingwa huo kwa sababu imeonyesha kuwa na mapungufu mengi licha ya kufika hatua hiyo ya robo fainali.
“Hii siyo Brazili ile ambayo tulikuwa tunaifahamu ambayo huiwezi kumaliza dakika 90, pasipo kutikisa nyavu za wapinzani tumeshuhudia mechi mbili ile ya
Mexico na Chile,ikimaliza bila ushindi siyo jambo zuri kwa sababu penalty ni bahati,”alisema Madaraka.
Madaraka alisema kocha Luis Fillipe Scolar,ameshindwa kufanya uchaguzi mzuri wa wachezaji kama alivyofanya mwaka 2002,wakati alipochukua ubingwa wa dunia kwa mara ya tano Korea Kusini na Japani.
“2002 alifanya uteuzi wa wachezaji sahihi na kupata timu ambayo ilikuwa ikiogopewa lakini inaonyesha mwaka huu amechemka hata ushindi wao ni kama wa kubahatisha na mbaya zaidi wapo nyumbani Scolari anapaswa kuwa makini,”alisema Madaraka.
Mkongwe huyo alimalizia kwa kuisifia timu ya Uholanzi ambayo imekuwa ikifanya vizuri tangu kuanza kwa michuano hiyo na kusema kama itaendelea hivyo inaweza kufuta machungu ya mwaka 2010 na kutwaa taji hilo.
Source:goal.com



0 comments:

Post a Comment