Wednesday 7 August 2024

GREEN BOY MR ONE TOUCH

Miaka kadhaa nyuma kabla ya 2018 dhahabu hii iliishia kupotelea mchangani hakuna aliyejali wala Kujaribu kuitazama Kwa jicho la thamani mpaka pale majeshi ya Vibes kutoka T-Motion Entertainment yapotumwa kwenda kuichimbua dhahabu hii.
Haikuwa kazi rahisi kukubalika na kupata nafasi ndani ya taasisi kubwa ya T-Motion Entertainment pamoja na kwamba alikuwa ni mshirika wao wa karibu pia kuwa mshikaji wa karibu na msanii wao namba Moja kipindi hicho Meshamazing.
Energy, Vibes,creativity na spirit vinamfanya kuwa ndiye Best Male Artist wa Mbeya currently mpaka pale atakapokuja kupatikana mwingine maana tangu ametangazwa na kwenye tuzo za MBEYA FINEST AWARDS 2020 (anavyodai yeye mwenyewe)
Mabibi na Mabwana namleta kwenu Green Boy 'Wizard' msanii mkali wa kizazi kipya anayefanya mitindo aina zote ya muziki ambaye alianza kama msanii wa muziki wa utamaduni wa HIP HOP 
Swali: Ilikuwaje ukabadilika kutoka kuwa msanii wa muziki wa HIP HOP ambao tulizoea kukuona kwenye vilinge kibao vya HIP HOP mpaka Sasa unaonekana unafanya sana bongo fleva music?
Green Boy: kiukweli hii ilikuja kipindi nimepewa nafasi ya kuwasilisha ngoma Kwa uongozi Kwa ajili ya kuipeleka media nikawasilisha ngoma zaidi ya tatu nilizokuwa naziamini sana wakazipokea nakuzisifia lakini hawakufanya chochote basi kuna siku boss alipita studio akasikia kuna ngoma tulikuwa tunafanya pale studio na haikuwa kwenye mipango basi boss akamwambia producer malizia hiyo kazi nataka. 
Basi producer kesho yake akaimaliza akampatia boss then boss akaniambia nikapige picha Kwa ajili ya kutengeneza cover la wimbo na siku iliyofuata nikapewa ratiba ya interviews redio mbalimbali. Hivyo ndivyo wimbo wangu wa kwanza CHUCHUMAA uliokuwa na mahadhi 'danso hiphop' ulivyobadilisha kila kitu kwenye safari yangu ya muziki maana ulipokelewa vizuri sana na hadi ikapelekea kidogo Boss na father Lugombo kidogo kutupiana lawama maana Lugombo aliamini kwasababu boss ana wasanii wa pure bongo fleva basi kanilazimisha na mimi niende kwenye mlengo huo. Baada ya ChuchuMaa nikaja na Moja namba,Ngabhaghila ft Mwaisa Nyonyoma,ChapChap n.k
Swali: Wanakuita Mzee wa one touch yaani ukaingia tu Tmotion halafu Ngoma Moja tu ukaingia mainstream?
Green Boy: Si mchezo,iko hivi kaka,kabla ya kuingia Tmotion nimepita machimbi kibao na vilinge vingi sana...watu wengi wanadhani hivyo...mimi nimesota sana pale Tmotion sio chini ya miaka miwili ndio nikakubaliwa then baada ya hapo nikawasilisha ngoma nyingi kwa uongozi mpaka ikakubaliwa ChuchuMaa kuanza nayo lakini pia baada ya ChuchuMaa nilipigishwa featuring nyingi sana na wasanii wengine ili nipate uzoefu wa kutosha.
Green Boy ni mmoja ya wasanii walioteuliwabkwenye BIG20 Mbeya 
Itaendelea...
- Maisha yake pale Tmotion 
- Safari yake south Africa 
- Ushkaji wake na Meshamazing 
- n.k
Imeandikwa na kizz1

3 comments: