Thursday, 3 April 2025

EASTER COMEDY SHOW: DONDOO MUHIMU KWA WALIOTAYARI KWA SHOW!

Hongera kwa kuwa mmoja wa mashabiki waliowahi kukata tiketi kwa EASTER COMEDY SHOW! Sasa kwa kuwa umehakikisha nafasi yako, hapa kuna vidokezo vya mwisho ili kuhakikisha unapata uzoefu wa kipekee siku hiyo:

1. HIFADHI TIKETI YAKO VIZURI

Hakikisha umeiweka tiketi yako mahali salama, iwe ni tiketi ya kawaida, VIP, Special Seat, au Meza ya watu 5. Ikiwa ni e-ticket, screenshot au print nakala ili kuepuka matatizo ya mtandao siku ya show.

2. PANGA MUDA WAKO – FIKA MAPEMA

Show inaanza saa 12:30 jioni na itaendelea hadi saa 5:59 usiku. Kufika mapema kutakusaidia:

- Kuepuka foleni ndefu

- Kupata nafasi nzuri ya kukaa (kwa wale wa Regular Tickets)

- Kujipanga kwa ajili ya burudani kamili

3. VAA MAVAZI MAZURI NA YALIYO NA MWELEKEO WA VICHEKO

Hii ni show ya kipekee, hivyo vaa kitu ambacho kinakufanya ujisikie huru na unaelekea kwenye tamasha kubwa! Ikiwa uko kwenye Regular, VIP au Special Seat, unaweza pia kwenda na muonekano wa kimaridadi kidogo kwa vibes nzuri.

4. ENDA NA MOOD YA KUCHEKA – USILETE STRESS!

Hii ni siku yako ya kufurahia na kicheko, kwa hiyo jiandae kwa burudani ya kiwango cha juu! Pumzika, acha stress zote nyumbani, na ujue kuna vichekesho vitakavyokufanya usahau matatizo yote kwa muda!

5. NJOO NA MARAFIKI AU FAMILIA – BURUDANI NI TAMU ZAIDI KWA PAMOJA!

Kama una nafasi ya kuja na rafiki au ndugu zako, itakuwa bomba zaidi! Meza ya watu 5 bado inapatikana, kama unataka kufanya booking ya kifamilia au na washikaji.

6. SHIRIKI NA WENGINE KWENYE MITANDAO!

Usisahau kushare excitement yako! Post kuhusu show, tumia hashtag kama:
#EasterComedyShowMbeya
#NjooUchekeMpakaMbavuZiiume
#StandUpComedyMbeya

Pia, fuata ukurasa wa Instagram kwa updates zote za mwisho  @standupComedy_mbeya

7. KUWA TAYARI KWA SUPRISE NA BURUDANI ZAIDI!

Mbali na vichekesho, kutakuwa na burudani nyingine za muziki, michezo midogo, na surprises kutoka kwa waandaaji! Jiandae kwa kitu spesho ambacho hakijatangazwa bado!

Siku inakaribia! Tunakutana TUGHIMBE HALL kwa show kali ya Pasaka!

1 comments: