HISTORIA NA UMUHIMU WA MBEYA TULIA MARATHON
Mbeya Tulia
Marathon ilianzishwa kama sehemu ya jitihada za kuhamasisha maisha ya afya na
kusaidia maendeleo ya jamii. Kwa miaka tisa sasa, mashindano haya yameendelea
kuwa moja ya matukio makubwa ya riadha nchini Tanzania, yakileta pamoja
washiriki wa rika na viwango mbalimbali, kutoka kwa wanariadha wa kulipwa hadi
kwa wapenzi wa riadha wa kawaida.
Lengo kuu la
marathon hii ni kutumia michezo kama nyenzo ya kuchangia maendeleo ya jamii.
Kila mwaka, sehemu ya mapato inayopatikana kupitia usajili wa washiriki
hutumika kusaidia miradi mbalimbali ya kuboresha miundombinu ya shule na vituo
vya afya, hasa katika Mkoa wa Mbeya na maeneo ya jirani.
KATEGORIA ZA MASHINDANO
Mbeya Tulia
Marathon 2025 itajumuisha kategoria tofauti za mbio, ili kutoa nafasi kwa
washiriki wa viwango vyote. Kategoria hizo ni:
-
Mbio ndefu – Kwa wanariadha wa hali ya
juu wenye uzoefu wa mbio ndefu.
-
Mbio za umbali wa kati – Chaguo bora kwa
wanariadha wa viwango vya kati na juu.
-
Mbio fupi – Kwa wale wanaopenda riadha
lakini hawajajiandaa kwa mbio ndefu,watu wa maofisini na watu maarufu.
-
Mbio za kasi – Zimeandaliwa kwa washiriki
wa rika mbalimbali, zikiwemo Watu maarufu, watu wa Maofisini,familia na
wanariadha wa makundi maalum.
JINSI YA KUJISAJILI
Washiriki
wote wanahimizwa kujisajili mapema ili kupata nafasi yao katika tukio hili la
kipekee. Usajili unaweza kufanyika kwa kupiga simu namba +255 767 860 515 au
+255 763 828 271.
MANUFAA YA KUSHIRIKI
Mbali na
changamoto ya kimwili na ushindani wa kushinda zawadi, kushiriki katika Mbeya
Tulia Marathon kuna manufaa mengi, ikiwemo:
-
Kuchangia maendeleo ya jamii – Sehemu ya
mapato hutumika kuboresha shule na vituo vya afya.
-
Kujenga afya bora – Mbio hizi
zinahamasisha maisha yenye afya na kujenga utimamu wa mwili.
-
Kukuza mshikamano wa kijamii – Washiriki
wanapata nafasi ya kukutana, kushirikiana, na kujifunza kutoka kwa wenzao.
-
Kutangaza utalii wa Mbeya – Mbeya ni
mojawapo ya maeneo mazuri zaidi nchini Tanzania, na marathon hii huleta wageni
wengi kutalii na kuchangia uchumi wa eneo hilo.
Mbeya Tulia
Marathon 2025 si tu mashindano ya riadha bali ni harakati ya maendeleo ya jamii
kupitia michezo. Ikiwa unataka kuwa sehemu ya historia, jiandikishe sasa na
ujiunge na maelfu ya wakimbiaji katika safari hii ya kuboresha maisha kupitia
riadha.
#TwendeMbeya
#MbeyaTuliaMarathon2025 #TunaboreshaMiundombinuYaElimuNaAfya #JisajiliSasa
0 comments:
Post a Comment