Katika tasnia ya muziki wa Injili, kuna majina machache yanayojitokeza kwa ubora, ubunifu, na uaminifu katika utumishi. Moja ya majina hayo ni Mixing Doctor kutoka Music Surgery, ambaye kwa neema ya Mungu amepata nafasi ya kipekee ya kuwania Tuzo Mbili katika Tanzania Gospel Music Awards (TGMA) 2025.
Kwa mwaka
huu, Mixing Doctor ameteuliwa katika vipengele viwili muhimu vinavyohusu upande
wa uzalishaji wa muziki:
- Muandaaji Bora wa Muziki wa
Injili wa Mwaka
- Mtayarishaji Bora wa Sauti wa Muziki wa Injili wa Mwaka
Hili ni
jambo la kujivunia si tu kwa Mixing Doctor binafsi, bali pia kwa wadau wote wa
muziki wa Injili nchini Tanzania na Afrika Mashariki kwa ujumla. Ubunifu wake
wa kipekee na kazi bora alizozifanya kwa wasanii wengi wa Injili zimempa nafasi
hii ya pekee.
NAMNA YA KUPIGA KURA
Ikiwa
unataka kumuunga mkono Mixing Doctor na kuonyesha kuthamini kazi yake
nzuri, fuata hatua hizi rahisi kupiga kura:
- Tembelea akaunti ya Instagram ya @mixingdoctor au @tanzaniagospelmusicawards
- Bonyeza link iliyopo kwenye
bio – itakupeleka kwenye ukurasa wa kupiga kura
- Chagua kipengele cha "Production
and Technical Awards"
- Tafuta na chagua vipengele viwili:
-
Muandaaji Bora wa Sauti wa Muziki wa Injili
wa Mwaka
-
Mtayarishaji Bora wa Muziki wa Injili wa
Mwaka
- Katika kila kipengele, chagua jina Mixing
Doctor
- Bonyeza Click to Vote chini
ya picha yake
- Ukiona ujumbe “You have voted for
Mixing Doctor”, basi kura yako imepita salama.
Uteuzi huu ni ushuhuda kwamba kazi njema haipotei bure. Mixing Doctor ameendelea kuwa msaada mkubwa katika kuboresha viwango vya uzalishaji wa muziki wa Injili na sasa anatambuliwa kitaifa.
Tuna nafasi
ya kumuwezesha kushinda kwa kumpigia kura. Tupige kura, tushirikishe
wengine, na tuendelee kuombea mafanikio ya huduma hii.
Mungu
akubariki sana kwa msaada wako.
0 comments:
Post a Comment