Sunday, 4 May 2025

KONGAMANO LA FUNDISMART LAFANYIKA KWA MAFANIKIO MAKUBWA JIJINI MBEYA

Mbeya, 29 Aprili 2025 – Kongamano kubwa la mafundi lilioandaliwa na FundiSmart chini ya uongozi wa Mkurugenzi Fredy Herbert Pole limefanyika kwa mafanikio makubwa, likihudhuriwa na zaidi ya washiriki 2,000 kutoka sekta mbalimbali za kiufundi na mnyororo mzima wa thamani wa kazi za ufundi nchini Tanzania.


UBUNIFU NA UONGOZI MADHUBUTI WA NDUGU FREDY POLE

Mafanikio haya yametokana kwa kiasi kikubwa na uwezo wa ndugu Fredy Pole kuongoza kwa ubunifu unaoleta matokeo chanya kwa jamii. Fredy amekuwa mstari wa mbele katika kuhakikisha mafundi wanapata nafasi ya kuonekana, kuunganishwa na fursa, na kubadilika kwenda kwenye mfumo rasmi wa kiuchumi.

Katika maandalizi ya kongamano hili, alihusisha makundi mbalimbali wakiwemo:

  • Vijana aliowalea na kuwapa ujuzi, ikiwemo katika sekta ya media
  • Wadau wa biashara na maendeleo aliyewahi kushirikiana nao
  • Watu wenye ushawishi katika jamii
  • Mafundi wa fani mbalimbali
  • Wafanya biashara
  • Serikali
  • Vyombo vya habari
  • Washiriki walioko kwenye mafunzo ya ufundi

MALENGO YA FUNDISMART

Katika hotuba yake, ndugu Fredy Pole alieleza malengo makuu ya FundiSmart kuwa ni:

  • Kuwaunganisha mafundi na fursa za kazi, zabuni na mitaji
  • Kuanzisha application ya mafundi kwa ajili ya masoko na mawasiliano
  • Kusaidia mafundi kurasimisha taaluma zao kwa kushirikiana na taasisi kama VETA
  • Kushawishi taasisi za kifedha kuwatengenezea mafundi huduma mahsusi

CHANGAMOTO ZINAZOWAKABILI MAFUNDI

Fredy pia aligusia changamoto kadhaa zinazowakabili mafundi, ikiwemo:

  • Gharama kubwa za kupata vyeti vya VETA
  • Ukosefu wa huduma maalum za kifedha kwa mafundi
  • Kutokuaminiwa kwa mafundi wazawa kwenye zabuni za serikali

KAULI ZA WADAU MUHIMU

MRATIBU WA VETA

  • Alisisitiza mafundi kufanya kazi kwa uadilifu na weledi
  • VETA ipo tayari kusaidia mafundi kurasimisha kazi zao
  • Gharama za usajili wa ujuzi zitapitiwa upya ili zisiwe kikwazo

    MKUU WA WILAYA YA MBEYA JIJI
  • Aliwataka mafundi kuwa waaminifu na wachukue tahadhari kazini
  • Aliahidi kufanyia kazi changamoto ya leseni za kazi na usajili kupitia EURA
  • Alipendekeza OSHA washirikishwe katika makongamano yajayo
  • Alihimiza mafundi kuwa na bima za afya
  • Alitoa wito kwa taasisi za kifedha kuunda huduma rafiki kwa mafundi
  • Aliwahimiza mafundi kuwapa thamani wadhamini wa kongamano

WADHAMINI WAKUU: LODHIA INDUSTRIES

Kampuni ya Lodhia Industries Ltd, ambao ndio wadhamini wakuu wa kongamano, walitoa fursa kwa mafundi kushirikiana nao kwa karibu zaidi. Wamefungua milango kwa mafundi kutembelea kiwanda chao kwa mafunzo, ushauri, na kuibua fursa mpya kupitia jukwaa la FundiSmart.

HITIMISHO

Kongamano hili limekuwa ni chachu ya mabadiliko makubwa kwa sekta ya ufundi Tanzania. FundiSmart imejidhihirisha kuwa daraja la kweli kati ya mafundi, soko la ajira, na taasisi mbalimbali za maendeleo. Ni dhahiri kuwa mafundi wa Tanzania sasa wana jukwaa sahihi la kuinua taaluma zao.

“FUNDI HUU NI WAKATI WAKO WA KUWA FUNDISMART!”

 

0 comments:

Post a Comment