MWANZO WA
SAFARI YA MUZIKI
Zuuh Winner alianza safari yake ya muziki mwaka 2023 kwa njia ya kipekee. Kabla ya kuingia rasmi katika kurekodi nyimbo zake, alijifunza muziki kwa kushiriki katika live band, jambo lililomsaidia kukuza uwezo wake wa kuimba na kuelewa uhalisia wa muziki wa jukwaani. Kupitia mazoezi katika bendi, aliweza kupata uzoefu wa moja kwa moja wa namna ya kuwasiliana na hadhira na kuimarisha uimbaji wake.
KUINGIA KWENYE KUREKODI NA KUACHIA E.P
Baada ya
kupata msingi mzuri katika muziki wa bendi, mwaka 2024 ulikuwa wa mafanikio
makubwa kwake. Alianza kurekodi kazi zake mwenyewe na hatimaye akaachia E.P
yake ya kwanza, hatua ambayo ilimpa nafasi ya kuthibitisha ubora wake kama
msanii wa kujitegemea. Kabla ya kuachia E.P, alijipatia mashabiki kwa kufanya cover
songs za wasanii wengine, ambazo zilimpa nafasi ya kujulikana na kupokelewa
vyema na mashabiki wa muziki.
WIMBO
MPYA "WEWE" FT. ICE MELOD
Kwa sasa, Zuuh Winner anatamba na wimbo wake mpya #Wewe, ambao amemshirikisha msanii Ice Melod. Wimbo huu unapatikana kwenye YouTube na majukwaa mengine ya muziki, na unazidi kumpa msanii huyu umaarufu zaidi katika tasnia ya muziki. Mashabiki wake wanaendelea kumpa sapoti kubwa, wakimpongeza kwa kazi nzuri na ubora wa sauti yake.
MWELEKEO
WA MUZIKI WAKE
Kwa jinsi
anavyokwenda kwa kasi, ni wazi kuwa Zuuh Winner ana mustakabali mzuri katika
muziki. Kujifunza kupitia live band na kuingia katika kurekodi rasmi ni
hatua muhimu zinazodhihirisha kuwa anajituma na ana dhamira ya kuwa msanii
mkubwa. Ubora wa kazi zake unaonekana wazi katika idadi ya wasikilizaji kwenye
majukwaa ya muziki, jambo linaloashiria kuwa bado ana mengi makubwa ya kutoa.
Kwa
mashabiki wa muziki wa kizazi kipya, Zuuh Winner ni jina la kufuatilia
kwa karibu. Kwa bidii yake, huenda akawa mmoja wa nyota wakubwa katika muziki
wa Afrika Mashariki.
Imeandikwa
na @mr_tee_kilaka_mashinee
#TunajivuniaZaidiVyaNyumbani
#ZuuhWinner
0 comments:
Post a Comment