Thursday, 17 April 2025

TASANIA YA MUZIKI MBEYA: VIPAJI VINAISHIA NJIANI KWA KIBURI NA DHARAU — SEHEMU YA PILI

Baada ya kuangazia changamoto ya wasanii pandikizi katika tasnia ya muziki mkoani Mbeya, sasa Robert anatuelekezea macho kwenye tatizo jingine kubwa ambalo limekuwa likiwazuia wasanii wenye vipaji kufikia mafanikio ya kweli ambalo ni 

KIBURI CHA KIPAJI, KUJIAMINI KUPITA KIASI, DHARAU NA KUKATAA USHAURI

Katika mazungumzo yetu na ndugu Robert ameeleza kuwaimebainika na kuthibitika kuwa vikwazo vikubwa vinavyowazuia wasanii wa Mbeya kutoka nje ya mkoa na kufikia mafanikio ya kitaifa au kimataifa licha ya vipaji vyao halisi ni:

KIBURI CHA KIPAJI NA KUJIAMINI KUPITA KIASI

Wasanii wengi wana vipaji vikubwa lakini mara tu wanapoanza kupata sifa chache kutoka kwa mashabiki wa mitaa yao, hujawa na kujiamini kupita kiasi kiasi cha kupuuza maoni na ushauri wa watu waliotangulia au wenye uzoefu zaidi. Hali hii huwafanya washindwe kuboresha kazi zao, kukataa kusikiliza wadau na mara nyingine hata kudharau fursa zinazotaka kuwakuza. Jambo hili ni tofauti kabisa na wasanii ambao wana vipaji na uwezo wa kawaida kwani wao wamekuwa wasikivu na kuzingatia ushauri na kufanyia kazi

DHARAU KWA WADAU NA WASANII WENZAO

Badala ya kushirikiana, kusaidiana au kujifunza kutoka kwa wenzao, baadhi ya wasanii wenye vipaji Mbeya wamejijengea tabia ya kuwakataa au/na kuwadharau wasanii wengine. Dharau hii pia huwafikia waandaaji wa matamasha, mapromota na hata maDJ ambao mara nyingi hushusha thamani ya msanii mwenye dharau anapojaribu kupenya kwenye majukwaa mapya na kumnyima fursa mpya zinapokuja kwa kuwa mara nyingi fursa nyingi kubwa na zenye hadhi na thamani  hupitia kwa watu hao.

KUKATAA USHAURI — NJIA YA KUJIANGUSHA

Tasnia ya muziki si kipaji pekee bali ni mchakato wa mafunzo endelevu. Msanii anayekataa kusikiliza ushauri wa watu waliopo mbele yake hujikuta akirudia makosa yale yale, kushindwa kubadilika kulingana na soko na hatimaye kutoweka kwenye ramani ya muziki.

ATHARI ZA TABIA HIZI KWA TASNIA YA MUZIKI MBEYA

-      Kipaji kinabaki mtaani — hata kazi nzuri hazivuki mipaka ya jiji au mkoa.

-     Mashabiki kupoteza imani — wasanii wanapojiona kama wako juu ya kila mtu, hata mashabiki huanza kupunguza sapoti.

-   Wadau hukwepa kushirikiana — hakuna mtu anayependa kushirikiana na msanii mwenye attitude mbaya.

-   Tasnia inakosa mshikamano — bila ushirikiano wa kweli, tasnia inakosa nguvu ya kujiinua mkoa mzima.

     NJIA ZA KUTOKA KWENYE MTEGO HUU

  1. Kujifunza Unyenyekevu na Nidhamu — Kipaji ni msingi, lakini tabia njema ndiyo daraja la mafanikio.
  2. Kukubali Ushauri — Mafanikio ni matokeo ya kujifunza kila siku kutoka kwa wadau, wanamuziki wenzako na hata mashabiki.
  3. Kujenga Mtandao wa Heshima na Ushirikiano — Mafanikio ya muziki hutegemea “teamwork”, si ubinafsi.
  4. Kujitoa kwenye fikra za ushindani wa kijinga — Ushirikiano wa kweli kati ya wasanii na wadau unaweza kuinua Mbeya kimuziki hadi nje ya mipaka.

Tasnia ya muziki wa Mbeya ina vipaji vingi, lakini wengi wao wamekuwa wakijifunga wenyewe kwa tabia za kiburi, dharau na kukataa ushauri. Hali hii imezuia mkoa kutoa wasanii wa nguvu katika soko la kitaifa na kimataifa.
Robert Eliah anaseme “Kipaji bila tabia ni sawa na gari bila mafuta — haikusafirishi popote.”

Kwa mabadiliko ya kweli, wasanii lazima wajifunze kwamba vipaji havitoshiTABIA, NIDHAMU NA USHIRIKIANO ndivyo vitakavyobeba ndoto.

0 comments:

Post a Comment