Mahali:
Tughimbe Hall, Mafiat – Mbeya
Tarehe:
Jumanne, 29 Aprili 2025
Muda:
Kuanzia saa 2:00 asubuhi
Kiingilio:
BURE kabisa!
MAFUNDI WANA NDOTO – FUNDISMART INAZITIMIZA
Katika
kongamano hili, FundiSmart inalenga kuwakutanisha mafundi kutoka sekta
mbalimbali kama vile:
-
Fundi umeme
-
Fundi kushona
-
Fundi uashi
-
Fundi bomba
-
Fundi magari
-
Fundi wa vifaa vya elektroniki
-
Fundi seremala, na wengine wengi
Kupitia
jukwaa hili, mafundi watapata nafasi ya kipekee ya:
KUJITANGAZA KITAIFA
Kwa kujiunga
na FundiSmart, mafundi wataweza kutangaza huduma zao na kuunganishwa moja kwa
moja na wateja kutoka maeneo mbalimbali ya nchi kwa njia ya kidigitali.
KUPATA CHETI CHA VETA
Fundi yeyote
anayefanya kazi ya ufundi bila kuwa na cheti rasmi, atapata nafasi ya
kuthibitishwa kitaaluma kupitia cheti cha VETA. Hii ni hatua muhimu kwa mafundi
wanaotafuta ajira, kandarasi za kazi au kushiriki zabuni za serikali na
mashirika binafsi.
KUJIFUNZA MBINU ZA KISASA
Mafunzo
maalum yataendeshwa kwa lengo la kuboresha ujuzi na maarifa ya mafundi ili
waweze kushindana katika soko la kisasa la ajira na huduma.
KUPATA MIKOPO NA BIMA
Kwa
kushirikiana na taasisi za kifedha, FundiSmart itawawezesha mafundi kupata
mikopo ya vifaa vya kazi, mitaji midogo, pamoja na huduma za bima kwa ajili ya
ulinzi wa maisha na kazi zao.
KUSHIRIKI MAKONGAMANO YA KITAIFA
Kwa kujiunga
na FundiSmart, mafundi wanapata fursa ya kualikwa kushiriki makongamano kama
haya yatakayokuwa yakifanyika katika mikoa mbalimbali, na hivyo kuwa sehemu ya
mtandao mpana wa kitaifa wa mafundi.
JINSI YA KUJIUNGA NA FUNDISMART
Mchakato wa
kujiunga ni rahisi na hauna gharama. Fungua simu yako kisha:
PIGA BURE *149*46*5# na fuata maelekezo.
Kwa mafundi
wanaotaka kujijengea jina, kuaminika zaidi, na kufungua milango ya mafanikio,
hii ndiyo nafasi yao adhimu.
Kongamano la
Mafundi Mbeya 2025 siyo tu tukio la kawaida – ni harakati ya mageuzi. Ni wakati
wa mafundi wa Tanzania kujifunza, kuthibitishwa, na kujiunga na dunia ya
kidijitali na kitaaluma kwa usaidizi wa FundiSmart.
“FUNDI HUU NI WAKATI WAKO WA KUWA FUNDISMART.”
Usikose tukio hili. Njoo, jifunze, jiinue – kwa pamoja tujenge Tanzania ya viwanda kwa mikono ya mafundi mahiri!
0 comments:
Post a Comment