Sunday 24 November 2013

Digital Media College of Tanzania.



Chuo kipo chini ya kampuni ya Radio Consult Limited na makao makuu yake ni Mbeya maeneo ya nanenane jengo la Chai.

Kwanini Digital Media College of Tanzania?
Kwasasa kuna vyuo vingi sana hapa nchini vinavyofundisha kozi hizi za media ukiwemo uandishi wa habari na utangazaji, changamoto kubwa iliyojitokeza ni kwamba wahitimu wote wanaomaliza katika vyuo mbalimbali wengi wao wanakosa ajira na kibaya zaidi wanashindwa kutumia elimu yao waliyoipata hata kujiajiri kwa kuandika habari, kumiliki mitandao (websites), kuandika na kuhariri vitabu, kutafuta fursa mbalimbali kwenye mitandao, kujiunga katika vyama mbalimbali ulimwenguni vinavyojihusisha na masuala ya uandishi wa habari, kuandaa makala na kushiriki kwenye mashindao mbalimbali. Kuna mambo mengi sana ambayo mwandishi wa habari anaweza kuyafanya bila kuajiriwa yaani namaanisha kwa kujiajiri mwenywe.

Hii ndiyo sababu kuu ambayo chuo cetu cha DMCT kinapenda kuiangalia kwamba kwa mwandishi wa habari yeyote yule kuanzia ngazi ya chini kabisa hadi ya juu wawe na uwezo wa kujiajiri wenyewe. Kuna tofauti kubwa kati ya nchi yetu na nchi za Africa Mashariki na Ulaya kwamba sisi mwandishi wa habari hutegemea ajira tu katika chombo cha habari na akikosa hpo anarudi kulala nyumbani na kulal mika hakuna ajira.

Katika kutafakari ni kwa njia zipi tutazitumia kumsaidia mwanafunzi au mwandishi wa habari aweze kujiajiri hata pale anapokosa chombo cha habari cha kufanyia kazi, DMCT tumeona ni bora tufundishe kozi zifuatazo kwa mwaka 2014:-
Certificate in digital Journalism kwa mwaka 1. Na
Certificate in Radio Production kwa mwaka 1.
Hii kozi ya digital journalism itawawezesha wanafunzi wote kuanza kutengeneza pesa hata kama ni kiasi kidogo wakiwa wanasoma kutokana na kazi za vitendo watakavyokuwa wanazifanya, kama kuandika habari na makala na kuziuza katika mitandao mbalimbali nje na ndani ya nchi. Pia watafundishwa masuala ya kumiliki mitandao (website na blog) kwa undani zaidi hali itakayowawezesha pia kuendelea kujipatia pesa. Vile vile kozi ya uandaaji wa vipindi ambayo itatoa waandaji wa vipindi wenye ujuzi wa hali ya juu ambao wanaweza hata kuuza vipindi vyao kwenye vyombo vya habari mbalimbali.

Details za chuo.
Uwezo wa kupokea wanafunzi: 50 tu kwa mwaka 2014.
Kozi: Certificate in digital Journalism
        Certificate in radio production.
Muda: Mwaka mmoja kila kozi atleast miezi 12 hadi 14. (miezi 2 ni English and computer course advanced course kuhakikisha kila mmoja anaweza kuongea English bila shida lakini pia anaweza kutumia computer bila shida, maana fursa nyingi zipo kwenye kiingereza na zinamtaka mtu awe na uzwezo wa kutumia computer) Miezi mingine 3 ni field na miezi iliyobaki ni masomo ya darasani na vitendo.
Uwiano wa mafunzo kwa vitendo: Chuo kinataraji kutumia mpaka 70% ya mafunzo kwa vitendo na 30% mafunzo ya nadharia.

Field tour: Tunatarajia kufanya filed tour mbalimbali kama
ifuatavyo:-
Field tour kutembelea chombo cha habari cha nje.Pia kutakuwa na tour mbalimbali kama kutembelea wakulima waliofanikiwa, kutembelea vyombo vya habari mbalimbali katika mikoa mbalimbali.

Mazingira ya kujifunzi: DMCT ina mazingira mazuri kwani mpaka sasa maandalizi yamekamilika Darasa la computer litakuwa na computer 20, pamoja na studio ya kisasa ya kujifunzia ambayo pia itatumika kwa kazi za kurekodi kwaya na mziki. Walimu mbalimbali wenye uzoefu watakuja kufundisha.
Ada: Kwa mwaka ni Tshs 600,000/= Laki sita tu au Dola 600 kwa wanafunzi kutoka nje. Malazi na chakula watajitegemea, lakini chuo kimewatafutia hostel kwa wanafunzi watakao taka kukaaa hostel.
                   Simu: 0718 114932 au 0763 099842 au 0686235888,
                    P o Box 2213 Mbeya.
                 Tunapatikana Nanenane Jengo la Chai RSTGA!

Kozi zingine tunazotarajia kuongeza baadaye ni:- Music Production, TV Production, ICT.

0 comments:

Post a Comment