Friday, 19 September 2025

MUZIKI UNAPOZUNGUMZA: WIMBO MPYA WA MESHACK FUKUTA ‘SILENCE’ WAACHWA HEWANI

‘Meshack Fukuta - Meshamazing (@amazing__tz), aendelea kuthibitisha kipaji chake kwa kuachia wimbo wenye hisia na ubunifu wa hali ya juu – SILENCE - sasa upo kwenye majukwaa yote ya kidigitali.’

Historia mpya imeandikwa rasmi katika muziki wa Tanzania pale jina la Meshack Fukuta, anayefahamika zaidi kama Meshamazing @amazing__tz, lilipotajwa mshindi wa mashindano makubwa ya kusaka vipaji vya kuimba nchini – Bongo Star Search (BSS) Msimu wa 10. Ushindi huu haukuwa tu furaha ya muda mfupi, bali umekuwa kumbukumbu isiyofutika kwa mashabiki wa muziki ndani na nje ya mipaka ya Tanzania.

ZAX AING’ARISHA MBEYA CITY DAY 2025

Mbeya, Septemba 6, 2025 – Mashabiki wa soka na wadau wa burudani jijini Mbeya walishuhudia tukio lisilosahaulika wakati msanii nyota wa muziki kutoka mkoani humo, Zax (@zax_4real2020), alipotoa burudani ya aina yake katika sherehe za Mbeya City Day 2025.

Wednesday, 10 September 2025

MWAFULANGO FC YAITEKA MBOZI - "Hatelele yazizima! Mwafulango FC yashusha soka safi la kisasa!Pasi 27"

Katika shamrashamra za kuelekea Sikukuu ya Mkutano Mkuu wa Ukoo wa Mwafulango unaotarajiwa kufanyika tarehe 6/9/2025, Ukoo wa Mwafulango kupitia idara yake ya michezo uliandaa mchezo wa kirafiki mnamo tarehe 5/9/2025 dhidi ya timu ya mpira wa miguu ya Hatelele Enjoy Soccer FC. Mchezo huo ulifanyika katika Uwanja wa Shule ya Msingi Hatelele na ulihudhuria na mashabiki lukuki walioteka uwanja huo.

AFYA YA AKILI KAMA MSINGI WA UBUNIFU NA USHINDI

Afya ya akili ni mhimili wa maisha ya kila binadamu, hasa kwa makundi yenye nafasi ya kipekee katika jamii kama wasanii na wanamichezo. Kupitia vipaji vyao, watu hawa huleta furaha, mshikamano, na mshangao kwa jamii. Hata hivyo, changamoto kubwa zinazowakabili mara nyingi hubaki kimya—changamoto za kisaikolojia.

Monday, 25 August 2025

WASANII NA WANAMICHEZO WASHIRIKIANA NA WATAALAMU KUELEWA CHANGAMOTO ZA AFYA YA AKILI

Kikao cha kina kilichohudhuriwa na wasanii, wanamichezo na wataalamu wa saikolojia kilijadili changamoto, suluhisho na njia za kuimarisha afya ya akili.

Jumapili, tarehe 24 Agosti 2025, ofisi za Wounded Healers Organization HQ – Forest Mpya, My Choice Street zilijaa shauku na hamasa wakati tukio la kwanza la “Uelewa wa Matatizo ya Akili kwa Wasanii na Wanamichezo” lilipofanyika. Kikao hiki kilijitahidi kutoa elimu, msaada na mwongozo kwa wasanii na wanamichezo kuhusu changamoto zinazohusiana na akili.