Mchakato wa kumpata mshindi katika Burudani Mbeya Awards umefuata hatua hizi:
1.
Kukusanya Kura
- Mashabiki
walipiga kura kwa njia ya mtandaoni (Google form).
- Kamati ya
wataalamu (academy) nayo imetoa kura zake kwa kutumia vigezo na taratibu.
2.
Kuhesabu Asilimia
Kwa kila
mgombea, hesabu zinafanyika kwa kutumia fomula hii:
-
Alama za Mashabiki = (Kura za mgombea ÷
Jumla ya kura za mashabiki) × 85
-
Alama za Academy = (Kura za mgombea ÷
Jumla ya kura za academy) × 15
-
Jumla ya Alama = Alama za Mashabiki +
Alama za Academy
3. Kupata
Mshindi
Mgombea
mwenye jumla ya alama nyingi zaidi ndiye anayeshinda tuzo husika.
Mfano wa Hesabu kwa Washindi wa Burudani Mbeya Awards
Ili kuelewa
vizuri jinsi washindi wa Burudani Mbeya Awards wanavyopatikana, tuangalie mfano
wa mgawanyo wa kura kwa wagombea watatu kwenye kategori ya Msanii Bora wa
Mwaka:
Mgombea |
Kura
za Mashabiki |
Kura
za Academy |
A |
10,000 |
30 |
B |
7,000 |
50 |
C |
5,000 |
20 |
Hesabu
kwa Mgombea A:
-
Alama za Mashabiki = (10,000 ÷ 22,000) ×
85 = 38.64
-
Alama za Academy = (30 ÷ 100) × 15 = 4.5
-
Jumla ya Alama = 43.14
Hesabu
kwa Mgombea B:
-
Alama za Mashabiki = (7,000 ÷ 22,000) ×
85 = 27.05
-
Alama za Academy = (50 ÷ 100) × 15 = 7.5
-
Jumla ya Alama = 34.55
Hesabu
kwa Mgombea C:
-
Alama za Mashabiki = (5,000 ÷ 22,000) ×
85 = 19.32
-
Alama za Academy = (20 ÷ 100) × 15 = 3
-
Jumla ya Alama = 22.32
Katika mfano
huu, Mgombea A ndiye mshindi kwa kuwa ana 43.14 alama, akifuatiwa na B
(34.55) na C (22.32).
UMUHIMU WA MFUMO HUU KATIKA BURUDANI MBEYA AWARDS
Mfumo huu
umehakikisha kwamba:
mashabiki wanakuwa na nguvu kubwa ya
kuamua mshindi, kwa kuwa kura zao zinachangia 85% ya alama.
Ubora wa kazi unazingatiwa,
kwani wataalamu wa burudani wanatoa maoni yao kwa kutumia vigezo vya kitaaluma.
Matokeo yanakuwa ya haki na yenye
uwazi, kwa sababu kila mgombea anapata nafasi sawa ya kushindania tuzo.
Tukutane April
2025 kwa utaratibu zaidi wa utangazaji wa washindi kwenye kila Category.
@BURUDANI MBEYA
0 comments:
Post a Comment