Katika maadhimisho ya kutambua vipaji vilivyoleta hamasa, ubunifu na mafanikio kwenye tasnia ya muziki mwaka 2024, msanii Smile Kiss ameibuka mshindi wa tuzo ya Mwanamuziki wa Kike Aliyefanya Vizuri katika Burudani Mbeya Awards 2025.
SAFARI YA MAFANIKIO
Mwaka 2024 ulikuwa wa mafanikio makubwa kwa Smile Kiss. Akiwa na sauti ya kipekee, msanii huyu ameweza kujiweka katika ramani ya muziki kwa kutoa nyimbo kali zilizogusa hisia za mashabiki, kupenya kwenye vyombo vya habari, na kufanikisha maonesho mbalimbali ya ndani na nje ya mkoa wa Mbeya.
Nyimbo zake
ziliendelea kupendwa mitandaoni, redioni, na katika majukwaa ya matamasha
mbalimbali, huku akionesha ukuaji wa kisanii na ukomavu katika maudhui, sauti,
na mawasiliano ya jukwaani.
SIFA ZA USHINDI
Smile Kiss
alishinda tuzo hii kupitia mchanganyiko wa kura za mashabiki (asilimia 85) na
alama kutoka kwa jopo la academy (asilimia 15), ambapo aliibuka na jumla ya
alama nyingi zaidi kutokana na:
-
Kazi nyingi na zenye ubora alizotoa 2024
-
Uwepo wake wa mara kwa mara kwenye matukio ya
burudani
-
Ushirikiano na wasanii wengine na kujenga
mahusiano ya kisanaa
-
Ushawishi wake kupitia mitandao ya kijamii
- Mwelekeo wake katika kutia moyo wasanii wa kike wengine
Smile Kiss anaendelea kuwa alama ya nguvu ya mwanamke katika sanaa. Ushindi wake si tu heshima kwake, bali pia ni mwanga kwa wasanii wengine wa kike kuamini kuwa juhudi, nidhamu na ubunifu hulipa.
BURUDANI MBEYA AWARDS
2025 – KUKUTAMBUA NI HESHIMA YETU.
💥💥💥smile kiss🔥
ReplyDelete