Msanii mahiri wa kizazi kipya, Zax 4Real, ametwaa tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kiume katika Burudani Mbeya Awards 2025, ikiwa ni kutambua mafanikio makubwa aliyoyapata mwaka 2024 ambao umejulikana kama mwaka wa kilele cha mafanikio katika safari yake ya muziki.
MWAKA WA MAFANIKIO
Mwaka 2024 umefungua ukurasa mpya kwa Zax
4Real. Akiwa na bidii, maono makubwa na uthubutu wa kisanii, amefanikisha mambo
kadhaa yaliyojenga msingi imara wa jina lake katika tasnia ya muziki wa Nyanda
za Juu Kusini na Tanzania kwa ujumla. Miongoni mwa mafanikio hayo ni:
-
Kuachia nyimbo kadhaa zilizopokelewa vyema na
mashabiki
-
Kuzindua EP na album, zilizodhihirisha ukuaji
wake wa kisanaa
-
Kufanya matamasha mengi ya mialiko katika mikoa
mbalimbali
-
Kuandaa shows zake binafsi, hatua
inayodhihirisha ujasiri na uimara wake kama msanii anayejitegemea
- Kuwa msanii aliyeongoza kwa kufanya shows nyingi zaidi Nyanda za Juu Kusini kwa mwaka 2024
MCHANGO KWA TASNIA
Zax 4Real ameonekana kuwa si tu msanii,
bali mfano wa kuigwa kwa wasanii wengine chipukizi. Ameonesha kuwa mafanikio
hayawezi kusubiriwi bali yanatafutwa kwa juhudi, ubunifu na kujitoa kwa
mashabiki. Kupitia muziki wake, amekuwa sauti ya vijana, na kupitia jukwaa
lake, amekuwa alama ya uthubutu wa kisanaa.
KAULI YA KAMATI
Kamati ya Burudani Mbeya Awards imemtaja
Zax 4Real kama msanii aliyestahili tuzo hiyo kwa kuwa:
“Amevuka mipaka ya kuwa msanii wa mtaani kuwa msanii wa jukwaa. Ametumia kila nafasi kubadilisha muziki wake kuwa harakati, burudani kuwa biashara, na ndoto kuwa uhalisia.”
Tuzo ya Mwanamuziki Bora wa Kiume kwa Zax 4Real ni ushahidi kuwa juhudi haziendi bure. Ushindi wake umeandika historia mpya katika Burudani Mbeya Awards, na kwa mashabiki wake, hii ni tuzo ya matumaini mapya, muziki bora zaidi, na mafanikio yasiyoisha.
BURUDANI
MBEYA AWARDS 2025 – KUKUTAMBUA NI HESHIMA YETU.
Ana stahili
ReplyDelete