Saturday 1 June 2013

SIFA SITA ZA WANYAKYUSA


1)WANAAMINI KABILA LAO NDIO BORA KULIKO YOTE
      Wanaamini kabila lao ni bora kuliko yote na ni lazima kila Mtanzania ajue kabila hilo na kama kuna mtu ambaye halijui basi mtu huyo ni jeuri/kiburi pia ana dharau.
2)WANAJIAMINI SANA
        Ni watu wanaojiamini sana hususani sehemu za kazi,wakipewa jukumu fulani kulifanya wanafanya kwa kijiamini sana na huwa hawapendi kuingiliwa 'as long as umempa afanye kitu fulani wanaamini kuwa umemchagua/umemteua yeye sababu unaamini kuwa anaweza kufanya kitu hicho so asiingiliwe mpaka amalize.

3)WANAPENDA ATTENTION
         Ni watu wanaopenda sana kuonekana kwa kile wanachokifanya,yaani wanapenda kuonekana na kuthaminiwa kwa kile wanachokifanya na sio zaidi ya hapo tofauti na makabila mengine.
4)NI WACHAPA KAZI
         Ni watu wanaojituma sana katika kufanya kazi,mara zote huwa hawapendi kuonekana kazi fulani imewashinda kufanya kwasababu wao wanaamini kuwa kushindwa kuperform vizuri kitu ulichoaminiwa ni AIBU na UDHAIFU mkubwa sana katika maisha.
5)WAKARIMU
       Ni watu walioumbwa na karima ya hali ya juu,yaani wanapokea mtu yoyote hata kama hawajui alikotokea ndio kitu kilisababisha mpaka kukawa na matukio ya ajabu ajabu sababu ukarimu huo watu wenye nia mbaya waliutumia katika kufanyia maovu yao.
6)WANASUBIRA
        Ni watu ambao hawana papara,huwa hawapendi kukurupuka kwa kitu chochote,wanapenda kungojea mpaka mpaka wapate hali halisi ya kitu chenyewe ndio wafanye maamuzi.

SIFA ZA ZIADA
a)UTANASHATI
      UTANASHATi na usafi ni sifa nyingine muhimu kwa kabila hii. Waweza fika kijijini ukakuta bibi na kijumba chake lakn vyombo vyake viko safi kabisa. Wawezakupataka chungu anachopikia usipate masizi
b)HAKI NA SHERIA
       Wanyakyusa kwa malezi yao WANAPENDA HAKI NA KUFUATA SHERIA.
C)UMOJA
         UMOJA ni sifa nyingine ya msingi: Si msibani tu Wanyakyusa wakoPAMOJA sana kwa kila kitu. Hata mgonjwa akisafirishwa hadi kwa mganga au hospitali kwa kushirikiana (palutato) wanashirikiana pamoja, Uzalishaji mali ndiyo usiseme- Walilima/wanalima kwa pamoja (INDUULA/INDIMYA), na ng'ombe walichunga/wanachunga pamoja (ULUTIIMO),mambo ya furaha kama harusi ndo usiseme,yaani wanahakikisha kwa umoja wao sherehe inafana.

3 comments:

  1. UTANASHATi na usafi ni sifa nyingine muhimu kwa kabila hii. Waweza fika kijijini ukakuta bibi na kijumba chake lakn vyombo vyake viko safi kabisa. Wawezakupataka chungu anachopikia usipate masizi

    ReplyDelete
  2. UMOJA ni sifa nyingine ya msingi: Si msibani zama hizo Wanyakyusa walikuwa PAMOJA sana. Hata mgonjwa alisafirishwa hadi kwa mganga au hospitali kwa kushirikiana (palutato), Uzalishaji mali ndiyo usiseme- Walilima kwa pamoja (INDUULA/INDIMYA), na ng'ombe walichunga pamoja (ULUTIIMO)...

    ReplyDelete