Katika mwendelezo wa kutambua vipaji na juhudi za wasanii na wadau wa sanaa wa Nyanda za Juu Kusini, Jay Wilz kutoka Black Dot Music ametangazwa kuwa Mtayarishaji wa Muziki (Music Producer) Aliyefanya Vizuri Zaidi katika Burudani Mbeya Awards 2025.
SAFARI YA KITAALUMA: KUTOKA ELSHADAI RECORDS HADI BLACK DOT MUSIC
Jay Wilz alianza kujulikana rasmi mwaka 2015, kupitia studio za Elshadai Records iliyopo Forest Mbeya, ambapo aliweka msingi imara wa kazi yake ya utayarishaji muziki. Ubunifu na usikivu wake wa kitaalamu vilimtofautisha mapema, na kumpa nafasi ya kushirikiana na vipaji vinavyochipukia.
Baadaye alihamia Black Dot Music iliyopo
Nzovwe, Mbeya – hatua ambayo ilikuza zaidi jina lake na kumpa fursa ya kufanya
kazi na wasanii wakubwa ndani na nje ya Tanzania. Ndani ya studio hizi, Jay
Wilz amekuwa sehemu ya uzalishaji wa hits mbalimbali zilizotikisa anga la
muziki.
KAZI NA USHAWISHI
Jay Wilz ametayarisha kazi za wasanii
mbalimbali kutoka Mbeya, mikoa ya Tanzania na hata nje ya nchi, akionesha:
-
Uwezo mkubwa wa kubadilika na kuendana na ladha
za muziki tofauti
-
Ubunifu unaokidhi viwango vya kitaifa na
kimataifa
- Nidhamu ya kazi na ushirikiano mzuri na wasanii
Wasanii wengi wamemuelezea Jay Wilz kama
mtayarishaji anayeelewa sanaa na heshima ya mchakato wa muziki, na ndio maana
amekuwa chaguo la kwanza kwa wengi.
USHINDI UNAOSTAHILI
Kwa mfumo wa kura uliotumika – asilimia 85 kutoka kwa mashabiki na 15 kutoka kwa academy – Jay Wilz aliibuka na alama nyingi zaidi, kuashiria kutambuliwa si tu na wataalamu, bali pia mashabiki waliothamini kazi yake kwa mwaka 2024.
Ushindi wa Jay Wilz ni ushahidi kuwa nyuma ya kila muziki mzuri, kuna mikono ya dhahabu isiyoonekana mara moja – na mikono hiyo leo imetambuliwa rasmi. Jay Wilz ameweka historia na kuonesha kuwa Nyanda za Juu Kusini zina utajiri mkubwa wa vipaji vya kiufundi katika muziki.
BURUDANI MBEYA AWARDS
2025 – KUKUTAMBUA NI HESHIMA YETU.
0 comments:
Post a Comment