Salum Juma Langa alihitimu masomo yake ya uanahabari mwaka 2017 na mwaka huo huo alianza rasmi safari yake ya kazi katika kituo cha redio Bomba FM. Hata hivyo, kabla ya
hapo, alifanya kazi katika Sweet FM kama mtangazaji wa vipindi vya burudani.Licha ya kuwa na ndoto ya kuwa mwanamuziki, mapenzi yake kwa tasnia ya habari yalimsukuma kuwa mtangazaji, akichukua fursa ya kipawa chake cha sauti na uwezo wa kuzungumza kwa ufasaha. Katika safari yake, alihamasishwa na watangazaji wakubwa kama Salim Kikeke wa BBC, na kwa sasa anapata motisha kutoka kwa majina makubwa kwenye vyombo vya habari vya kidigitali kama Sky na Millard Ayo.
VYOMBO
VYA HABARI ALIVYOFANYIA KAZI
Katika safari yake ya kazi, Vocalizer amepitia vyombo mbalimbali vya habari, akianza kama mtangazaji wa vipindi vya burudani katika Sweet FM, kisha kuhamia Bomba FM ambako alifanya kazi si tu kama mtangazaji wa burudani, bali pia wa vipindi vya habari na michezo, na hatimaye kuwa Mkuu wa Vipindi katika kituo hicho. Aidha, alipata
nafasi ya kushirikiana na BBC Swahili kama mwandishi wa habari kutoka Mbeya.SAFARI YA
KUANZISHA SDP UPDATES
Baada ya miaka ya kujifunza na kupata uzoefu katika vyombo vikubwa vya habari, Vocalizer aliamua kuanzisha SDP UPDATES, chombo cha habari cha kidigitali kinacholenga kusambaza habari, burudani, na vipindi mbalimbali kwa njia ya mtandaoni. Alisema kuwa
mabadiliko ya kidigitali na upungufu wa majukwaa ya kidigitali yanayoshughulikia sanaa katika Nyanda za Juu Kusini vilimsukuma kuanzisha SDP UPDATES.Licha ya
kuwa kiongozi katika Bomba FM, uamuzi wa kuacha nafasi hiyo haukuwa
rahisi. Hata hivyo, aliona ni wakati wake wa kujitegemea na kujenga jina lake
kupitia chombo chake cha habari. Hadi sasa, anajivunia mafanikio makubwa
kupitia SDP UPDATES, huku akiamini kuwa juhudi zake, pamoja na msaada wa timu yake,
zitalifanya kuwa chombo namba moja cha habari katika Nyanda za Juu Kusini.
MAFANIKIO
NA CHANGAMOTO
Kupitia kazi yake ya uwanahabari, Vocalizer amepata mafanikio mengi, ikiwa ni pamoja na
kufahamika zaidi, kujenga mtandao wa watu, na kupata kipato kupitia chombo chake cha habari. Ameweza pia kusaidia vijana zaidi ya kumi kujifunza kazi ya uwanahabari na kuwapa mwanga wa kuendelea katika tasnia hiyo.Changamoto
kubwa aliyokumbana nayo ni wakati wa kujitambulisha kwenye tasnia, ambapo
ilimchukua muda kupata uaminifu wa watu. Hata hivyo, kwa juhudi na uvumilivu,
alifanikiwa kujijenga na kuleta mabadiliko chanya katika kazi yake.
HABARI NA MAHOJIANO YANAYOMPA FAHARI
Kati ya mahojiano mengi aliyowahi kufanya kupitia SDP UPDATES, Vocalizer anajivunia sana mahojiano yake na
Young Lunya, ambapo aliweza kusaidia kumtambulisha kijana mdogo kutoka Mbeya aitwaye Danny Lunya kwa hadhira ya Tanzania nzima. Anasema kuwa mahojiano haya yalileta mafanikio makubwa na ni moja kati ya kazi zake alizojivunia zaidi.USHAURI
KWA VIJANA
Kwa vijana wanaotaka kujiingiza katika tasnia ya habari na burudani, Vocalizer anawashauri wawekeze nguvu kwenye sekta ya kidigitali, kwani dunia inakwenda kasi sana na kuna fursa nyingi za kujipatia kipato kupitia majukwaa ya mtandaoni. Pia anawahimiza kuwa wavumilivu, kwani mafanikio hayaji kwa usiku mmoja bali yanahitaji
muda, mchakato na uvumilivu.HITIMISHO
Safari ya
Salum Juma Langa a.k.a Vocalizer ni mfano halisi wa jinsi nidhamu, bidii, na
kutumia fursa za kidigitali vinavyoweza kubadili maisha ya mtu na kumfikisha
mbali. Kupitia SDP UPDATES, anaendelea kuleta mapinduzi katika tasnia ya
habari, huku akiwahamasisha vijana wengi zaidi kujiingiza katika uwanja wa
habari na burudani kwa kutumia teknolojia ya kisasa.
Burudani
Mbeya Media inamtakia kila la heri katika safari yake ya uwanahabari na
maendeleo ya SDP UPDATES.
0 comments:
Post a Comment