Thursday 16 November 2023

AMMY CHIBA MSINGI WA T-MOTION ENTERTAINMENT

AMMY CHIBA MSINGI WA T-MOTION
Kutoka kwenye Instagram page rasmi ya T-Motion Entertainment wameandika haya

Pamoja na ukubwa aliokuwa nao Ammy Chiba na uzoefu mkubwa aliokuwa nao kwenye tasnia ya muziki lakini alikuwa ndiye msanii namba moja kwa utii na kufuata maelekezo pia hakuacha kushauri pale alipoona panahitaji ushauri kwa uzoefu aliokuwa nao. 
Alikuwa ni msanii aliyekuwa anatamani na anataka Lebo ikue kubwa Zaidi ya ukubwa alio nao yeye,hapa nanukuu moja ya ushauri ambao alishawahi kuutoa.
‘Boss unajua ninapokuwa naonekana mimi tu LEBO haitakuwa…boss naomba niwashauri vitu viwili kama vitawezekana;-
Jitahidini kuhakikisha kunakuwa na Stori matukio mengi sana yanayohusu Lebo yetu yatakayokuwa yanaongelewa kwenye vyombo vya habari,mitandaoni,mitaani na kwenye lebo zingine
Msanii hapa nisiwe peke yangu ninayehangaikiwa,nashauri wasanii wengine hapa pia wakuzwe ingawa sio kwa mara moja inaweza ikaandaliwa program nzuri isiyoumiza kwa ajili ya kuwakuza wasanii wengine pia,hii itasaidia pia mimi kutokuzubaa na itanikomaza Zaidi lakini pia kunapokuwa na ushindani kwenye Lebo ndio viwango vya wasanii vinakuwa maana kila mmoja anakuwa anataka afanye vizuri ili awe kinara wa Lebo hivyo leo inakuwa na wakali watupu na ndipo inakua. So boss tuwakuze angalau wasanii wawili
HANA UBINAFSI
Alikuwa ni msanii anayewapigania sana wasanii wenzake ambao yupo nao Lebo na hata walio nje ya Lebo,alikuwa akiona kama kuna kitu ambacho kama lebo tunaweza kufanya kwa msanii Fulani mwenye uhitaji hakusita kutushawishi kukifanya lakini akitueleza na faida tutakazopata kwa kuweza kukifanya kitu hicho. Lakini pia kwa wasanii ambao walikuwa chini ya lebo hakusita kuwaelekeza vitu ambavyo alikuwa anavijua ili wakue ikiwemo namna ya kuishi kama msanii,namna ya kuishi na viongozi wako,namna ya kuishi na wasanii wenzako,namna ya kuishi na media,namna ya kuishi na wadau wote kiujumla pia kuwafundisha kuimba alifanya sana hiyo kazi kwa wasanii waliokuwa lebo bila kujali kuwa hawa nawafundisha lakini ndio washindani wangu kwenye kazi yake.

ITAENDELEA…
https://www.instagram.com/reel/Czs_G1VNX67/?igshid=NjZiM2M3MzIxNA==

0 comments:

Post a Comment