Tuesday 31 October 2023

Usipomtaja PRODUCER DAYO ‘Dayonga’ Kwenye Orodha Yako Maproducer Wako Bora Huendi Mbinguni

Tunaweza kuwaambia nini wasanii na watangazaji wapya kuhusu producer Dayonga?
Hilo ni swali kutoka instagram page maarufu kwa habari za burudani na mitindo nyanda za juu kusini inayojulikana kwa jina la DONDOSHA NEWS.
Baada ya post hiyo watu maarufu na mashuhuri Mbeya walikuja kuweka maoni yao kama ifuatavyo;
DjDebby – ‘Mtu na nusuu…Mali safi kabisa toka kwa mzee wetu Mwambigija
VicentLaurentjrr: - ‘Dayo brotherhood toka studio ikiwa Ilolo kule katengeneza music wa wengi hawajui aisee,akiwa na Zest ,Kikunizo kabla watu hawajamjua Zax4Real kulikuwa na Zax b pembeni Ammychiba,wewe huo muziki weka mbali kabisa na watoto wa 2000 kule Nzovwe kulikuwa na Gachi b anamsuka mtu kama Trio na Rayvanny wakati huo anaitwa Raymond halafu Tunduma kuna vijana wangu Shababi International halafu kuna vichwa kama Dk Fazi na kwenye Hip hop kuna kina Makanta’
DoctorFazi: - ‘Huyu jamaa ukisikia mtu ana bifu naye basi jua huyo mtu ndio mkorofi,Dayo ni Rasta mno’
Chazdax: - ‘Hanaga noma mara ya kwanza niliweza kujuana nae studio za Mashada inc pia alikuwepo na producer Losso pale’
Bossprota: - ‘Legends Dayo plus Losso pluss Kikunizo
Comic Cliff: - Aishi milele
Baada ya kuisoma hii post na comments zake timu nzima ya burudani Mbeya ikaamua kuingia chimbo kutaka kujua huyu Dayonga ni nani hasa?
Dayonga zamani akijulikana kama producer Dayo wa Mashada inc aliyeandaliwa na Godfather wa entertainment Mbeya boss Kikunizo baada ya Zest na Losso pale mashada inc Production.
Dayo anatokea kwenye familia ya watu maarufu yam zee David Mwambigija wa jijini Mbeya yenye ndugu zake wengine maarufu kama Kikunizo Montage, Creator Pro, Criss R7 na wengine
Dayo ni miongoni mwa producer wa mwanzo kabisa wazawa walioleta mapinduzi makubwa sana ya muziki Mbeya kwa kuweza kufanya kazi nyingi zenye viwango vya hali ya juu mpaka kusababisha wasanii wa ukanda huu wa nyanda za juu kusini waache kwenda kurekodi dar es salaam na kurekodi hapahapa Mbeya.
WASANII NA WATANGAZAJI WENGI WAPYA HAWAMFAHAMU HUYU JAMAA?
Vitu vingi vilimjia kwa pamoja na kwa haraka bila kuwa na utayari
Kuanzishwa kwa mashada photo point,ikumbukwe vision nzima ya mashada inc ni ya Kikunizo hivyo baada ya kuanzishwa kwa Mashada photo point akaamua kumuachia mdogo wake Dayo studio ya muziki na wakati huo uwezo wa Dayo kwenye kusimamia studio haukuwa mzuri sana maana ilitakiwa yeye mwenyewe asimamie studio halafu afanye production then asimamie artists,promotion n.k kitu ambacho kabla alikuwa anakifanya Kikunizo. 
Kwa kipindi cha kuanzia mwaka 2016 Dayo alipumzika kufanya kazi za muziki akawa anafanya shughuli zingine nje na muziki hivyo kizazi hiki cha kuanzia miaka hiyo imekuwa ngumu kidogo kumfahamu
Kwasasa Dayo ‘Dayonga’ yupo mjini Dar es Salaam akifanyakazi za muziki kwa kiwango kikubwa sana na studio kubwa na wasanii wakubwa. Zaidi tembelea insta page ya @dayonga_
Ukitaja majina matatu ya maproducer walioleta mapinduzi ya production Mbeya usisahau jina la Dayonga kwenye list yako,usipomtaja huendi mbinguni.
Credits: - DondoshaNews, VicentLaurent,DoctorFazi,Djdebby,Chazdax,Bossprota,Comic

0 comments:

Post a Comment