Kutoka kwenye mtaa hadi madhabahuni, kutoka kwenye midundo ya danso hadi ujumbe wa uzima, msanii aliyejulikana kama Green Boy, sasa anakuja kwa jina lenye uzito wa kiroho na msimamo wa kipekee Believer.
Na sasa, akiwa amezaliwa mara ya pili katika Kristo, Believer ameachia rasmi wimbo wake wa kwanza wa Injili unaoitwa “NIMEAMUA” kazi ya kwanza chini ya chapa yake mpya kama msanii wa muziki wa kiroho, aliyejitenga rasmi na maisha ya zamani na kuamua kusimama kwa ajili ya Bwana.