Katika mwendelezo wa kutambua mchango wa watu walioweka msingi na kuendeleza sanaa katika ukanda wa Nyanda za Juu Kusini, Omary Juma, maarufu kama DJ Speed, ametunukiwa rasmi Tuzo ya Heshima kwenye Burudani Mbeya Awards 2025 kwa mchango wake mkubwa kwenye tasnia ya muziki na katika fani ya U-DJ wa kisasa.
MWAKILISHI WA “GENERATION YA MAPINDUZI”
DJ Speed anawakilisha generation ya tatu
ya muziki, yaani kipindi cha miaka 2006 hadi 2015, kilichokuja baada ya
generation ya kwanza (1990–2000) na ya pili (2001–2005). Hii ni generation
iliyoleta mapinduzi ya kweli katika fani ya U-DJ na muziki kwa ujumla, hasa kwa
kuingiza teknolojia na mbinu mpya za kupromote muziki ndani na nje ya Mbeya.
Kupitia kipindi hicho, DJ Speed aliibuka
kama mmoja wa madj wa mwanzo kuhamisha fani ya U-DJ kutoka kwenye mitaa na
harusi hadi kwenye redio, kumbi kubwa za burudani, matamasha, na majukwaa ya
kitaalamu.
MCHANGO WAKE KWENYE TASNIA
Mwasisi wa Mbeya All Star: Mnamo mwanzoni
mwa miaka ya 2010, DJ Speed aliliasisi kundi hili muhimu lililowaleta pamoja
wasanii wa Mbeya kwa lengo la kushirikiana, kusaidiana na kuinua kazi zao na
kuisemea jamii kupitia muziki. Wimbo maarufu uliovuma sana kupitia Mbeya all
Stars uliitwa MBEYA NYUMBANI.
MWANZILISHI WA TEAMKAZI ENTERTAINMENT
Kupitia uongozi wake, DJ Speed alisimamia
na kukuza wasanii kadhaa wa Bongofleva, na pia aliwajengea nafasi madj
chipukizi.
PROMOTER NA MENEJA WA WASANII
Alikuwa Dj wa mwanzoni kuanzisha
utaratibu wa kuwapromote wasanii kupitia majukwaa ya kitaalamu na mitandao ya
kijamii, akiwapa shows, airtime kwenye redio, na usimamizi wa kisanaa.
MLEZI WA VIPAJI
Mojawapo ya sifa kubwa ya DJ Speed ni
uwezo wake wa kugundua na kulea vipaji, hasa kutoka kizazi cha tatu cha wasanii
wa Nyanda za Juu Kusini. Wengi wao wanamchukulia kama mlezi, daraja na nguzo ya
mafanikio yao ya kwanza kwenye muziki.
TUZO YA HESHIMA: USTAHILI ULIO DHAHIRI
Kwa kutumia ushawishi wake na uzoefu wa miaka mingi, DJ Speed ameacha alama isiyofutika katika ramani ya burudani. Tuzo ya heshima anayopokea mwaka huu ni uthibitisho wa jinsi alivyokuwa msingi imara wa ukuaji wa fani ya muziki katika mkoa wa Mbeya na maeneo jirani.
DJ Speed ni mfano wa wale watu wa nyuma ya pazia walioamua kutoa muda, nguvu na rasilimali zao kwa ajili ya kuinua wengine. Kwa kutambuliwa kwake, Burudani Mbeya Awards inaendeleza dhamira yake ya kuenzi historia, mchango na uzalendo wa kweli kwenye sanaa ya muziki.
BURUDANI MBEYA AWARDS
2025 – KUKUTAMBUA NI HESHIMA YETU.
No comments:
Post a Comment