MBEYA, TANZANIA
Baada yakipindi cha hamasa, kura, na matarajio makubwa, hatimaye wasanii, mashabiki, na wadau wa burudani wanakaribia kushuhudia kilele cha Burudani Mbeya Awards 2025. Kamati ya maandalizi imetangaza kuwa kutangazwa rasmi kwa washindi wa tuzo hizi kutaanza Jumatatu, tarehe 19 Mei 2025, kwa mtiririko maalum utakaoendelea hadi washindi wote kwenye vipengele vyote 26 watakapojulikana.
MFUMO WA
UPATIKANAJI WASHINDI
Mwaka huu,
Burudani Mbeya Awards imetumia mfumo wa uwazi na usawa, ambapo mshindi katika
kila kipengele alipatikana kwa kujumlisha alama zilizotokana na:
85% ya kura
za mashabiki, waliopiga kura kupitia mitandao na njia rasmi zilizowekwa, na
15% ya kura
kutoka kwa “academy” ya wataalamu wa sanaa na burudani, waliotathmini kazi za
wasanii kwa vigezo vya kitaalamu.
Mfumo huu
umehakikisha kwamba sauti ya mashabiki inasikika kwa nguvu huku pia ubora wa
kisanaa ukizingatiwa kikamilifu.
MCHAKATO WA KUTANGAZA WASHINDI
Katika
kuhakikisha kila mshindi anapewa nafasi ya pekee na kuthaminiwa ipasavyo,
washindi watatangazwa kwa awamu ya washindi watatu (3) kwa siku za kazi
(weekdays), kuanzia Mei 19 hadi watakapokamilika wote 26.
Tangazo la
mshindi mmoja litatolewa asubuhi,
mwingine mchana, na wa mwisho jioni.
Majina na
kazi za washindi zitapambwa kwa maelezo ya kazi waliyoshinda nayo, picha, video
na ujumbe wa shukrani kutoka kwao.
Njia za Kufuatilia
Mashabiki
wanahimizwa kufuatilia matokeo kupitia:
Burudani
Mbeya Blog – kwa habari rasmi na taarifa kamili za kila mshindi
Instagram:
@burudanimbeya – kwa picha na vipande vya ushindi
KAULI KUTOKA KWA KAMATI
Mratibu Mkuu
wa tuzo hizi amesema:
“Mwaka huu
tumeshuhudia vipaji vingi vikubwa, vilivyotoka kila kona ya Mbeya. Tunawapongeza
washiriki wote, na hasa washindi ambao wamepewa heshima hii kwa kura za
wananchi na tathmini ya kitaalamu. Tuzo hizi si mwisho, bali ni mwanzo wa
safari kubwa zaidi ya sanaa Mbeya.”
Kuelekea Katika Kilele
Burudani Mbeya Awards si tu jukwaa la tuzo, bali ni harakati ya kuinua na kuendeleza tasnia ya burudani katika mkoa wa Mbeya. Kwa mwaka huu, vipengele 26 vilivyoshindaniwa vimeakisi upana wa vipaji katika muziki, uigizaji, utunzi, sanaa ya picha, burudani za asili na nyingine nyingi.
Kama ulihusika
kupiga kura, au wewe ni shabiki wa kweli wa burudani ya Mbeya, huu ni wakati
wako. Fuatilia kila tangazo – asubuhi, mchana na jioni – ujue nani amebeba
heshima ya kuwa mshindi wa Burudani Mbeya Awards 2025.
BURUDANI MBEYA AWARDS – KUKUTAMBUA NI HESHIMA
YETU!
ππΎπͺπΎ
ReplyDelete